KAMATI ZA MAADILI ZA MAOFISA WA MAHAKAMA
Wajumbe
i.Jaji wa Mahakama ya Rufani ambayeatakuwa Mwenyekiti;
ii.Majaji watatu wa Rufani ambao watateuliwa na Mhe. Jaji Mkuu;
iii.Majaji watatu wa Mahakama Kuu watakaoteuliwa na Mhe. Jaji Mkuu.
iv.Msajili Mkuu ambaye atakuwa Katibu wa Kamati.
Wajumbe
i.Mhe. Jaji Kiongozi ambaye atakuwa Mwenyekiti;
ii.Majaji wawili wa Mahakama Kuu wanaoteuliwa na Mhe. Jaji Mkuu;
iii.Mahakimu wawili wanaoteuliwa na Mhe. Jaji Mkuu.
iv.Msajili wa Mahakama Kuu ambaye ni Katibu wa Kamati.
Wajumbe
i.Mkuu wa Mkoa ambaye ndiye Mwenyekiti;
ii.Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mkoa;
iii.Katibu Tawala wa mkoa;
iv.Wajumbe wawili watakaoteuliwa na Mkuu wa Mkoa kutoka miongoni mwa watu mashuhuri mkoani mwake;
v.Mahakimu wawili watakaoteuliwa na Jaji Mfawidhi kutoka katika mkoa au Wilaya husika.
- 4.KAMATI YA MAADILI YA MAAFISA WA MAHAKAMA YA WILAYA
Wajumbe
(i)Mkuu wa Wilaya ambaye ndiye Mwenyekiti;
(ii)Hakimu Mkazi wa Wilaya au Hakimu wa Wilaya Mfawidhi wa Wilaya husika;
(iii)Katibu Tawala wa Wilaya;
(iv)Wajumbe wawili watakaoteuliwa na Mkuu wa Wilaya, mmojawapo akiwa Kiongozi wa dini, ambao kwa maoni ya Mkuu wa Wilaya ni mwadilifu , mweledi na anao uwezo wa kushiriki katika majukumu ya Kamati.
(v)Mahakimu wawili watakaoteuliwa na Jaji Mfawidhikutoka Wilaya husika.