KAMATI ZA MAADILI ZA MAOFISA WA MAHAKAMA

Wajumbe

i.Jaji wa Mahakama ya Rufani ambayeatakuwa Mwenyekiti;

ii.Majaji watatu wa Rufani ambao watateuliwa na Mhe. Jaji Mkuu;

iii.Majaji watatu wa Mahakama Kuu watakaoteuliwa na Mhe. Jaji Mkuu.

iv.Msajili Mkuu ambaye atakuwa Katibu wa Kamati.

Wajumbe

i.Mhe. Jaji Kiongozi ambaye atakuwa Mwenyekiti;

ii.Majaji wawili wa Mahakama Kuu wanaoteuliwa na Mhe. Jaji Mkuu;

iii.Mahakimu wawili wanaoteuliwa na Mhe. Jaji Mkuu.

iv.Msajili wa Mahakama Kuu ambaye ni Katibu wa Kamati.

Wajumbe

i.Mkuu wa Mkoa ambaye ndiye Mwenyekiti;

ii.Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mkoa;

iii.Katibu Tawala wa mkoa;

iv.Wajumbe wawili watakaoteuliwa na Mkuu wa Mkoa kutoka miongoni mwa watu mashuhuri mkoani mwake;

v.Mahakimu wawili watakaoteuliwa na Jaji Mfawidhi kutoka katika mkoa au Wilaya husika.

Wajumbe

(i)Mkuu wa Wilaya ambaye ndiye Mwenyekiti;

(ii)Hakimu Mkazi wa Wilaya au Hakimu wa Wilaya Mfawidhi wa Wilaya husika;

(iii)Katibu Tawala wa Wilaya;

(iv)Wajumbe wawili watakaoteuliwa na Mkuu wa Wilaya, mmojawapo akiwa Kiongozi wa dini, ambao kwa maoni ya Mkuu wa Wilaya ni mwadilifu , mweledi na anao uwezo wa kushiriki katika majukumu ya Kamati.

(v)Mahakimu wawili watakaoteuliwa na Jaji Mfawidhikutoka Wilaya husika.