Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan (katikati) pamoja na Viongozi wengine walioketi wakiwa katika picha ya pamoja na Majaji wapya wa Mahakama ya Rufani mara baada ya kuapishwa kwao leo tarehe 26 Mei, 2026 Ikulu jijini Dar es Salaam. Wa tatu kushoto ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, wa tatu kulia ni Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju, wa pili kushoto ni Jaji Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Khamis Ramadhan Abdallah, wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka, wa pili kulia ni Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Mhe. Daniel Sillo (Mb) na wa kwanza kulia ni Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera.